skip to main
|
skip to sidebar
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Msingi na Sekondari na hataki kusikia kuwa wanafunzi wanarudishwa shuleni kwa ababu hawajalipa mchango wa chakula au dawati.
President JPM amewataka Mawaziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako na TAMISEMI Selemani Jafo kulisimamia hilo huku akiwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi nchi nzima kuhakikisha hakuna Shule ambayo inachangisha mchango wa aina yoyote huku akisema kwa yeyote atakataka kuchangia basi apeleke mchango wake kwa Mkurugenzi ambaye ataamua matumizi ya mchango huo kwa shule husika.
Hizi hapa habari kubwa zote ambazo zimepewa kipaumbele kwenye magazeti ya Tanzania leo January 17, 2018.
Chama cha Mawakili nchini Uganda kimefungua kesi katika Mahakama ya Katiba kupinga mabadiliko ya Katiba yanayoondoa ukomo wa umri wa mgombea Urais.
Muswada wa mabadiliko hayo umepitishwa na Bunge la nchi hiyo na tayari Rais Museveni amesaini kuwa Sheria.
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema ujumbe wa Rais Magufuli alipomuita Ikulu January 9, 2018 ulikuwa ni kumshawishi kurejea CCM lakini alikataa.
Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA amesema alimweleza Rais Magufuli kuwa hakubahatisha kufanya uamuzi wa kuhama CCM kwenda CHADEMA.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF ambayo ilikutana Jumapili January 14, 2018 imemfungia mechi 3 mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa.Mbali na kumfungia mechi tatu, pia imempiga faini ya Tsh 500,000 mshambuliaji huyo baada ya kukiri kumpiga mchezaji wa Tanzania Prisons wakati wa mchezo uliozikutanisha timu hizo November 25 ,2017.
Copyright © 2011.
The Chief
- All Rights Reserved.